Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
YAH: KADI YA MWENDOKASI KWA SHILINGI 1,000/- TU!
16 May, 2025

YAH: KADI YA MWENDOKASI KWA SHILINGI 1,000/- TU!

 

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) unautaarifu umma kuwa ili kusafiri kwenye mfumo wa DART, kila msafiri anapaswa kuwa na Kadi  ya Mwendokasi. Katika kuboresha huduma na mfumo wa ukusanyaji wa nauli pamoja na kuruhusu wateja wetu kutumia kadi, bei ya kadi hii imeshushwa hadi Sh 1,000/= (Yaani Shilingi  Elfu Moja tu) kuanzia tarehe 17 Mei, 2025.

 

Matumizi ya tiketi za karatasi yatafutwa rasmi ifikapo tarehe 30 Juni, 2025. Baada ya tarehe hiyo, wasafiri wenye kadi pekee ndio watakaoweza kusafiri kwa  kutumia mabasi ya mfumo wa DART.  Utaratibu wa matumizi ya kadi hautahusisha wanafunzi.

 

NUNUA KADI YA MWENDOKASI LEO, SAFIRI KWA HARAKA NA UHAKIKA!

 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka – DART
Tarehe
: 16 Mei, 2025