Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
Flora E. Nyanana photo
Flora E. Nyanana

Mkuu wa Kitengo cha Ubora na Usimamizi wa Vihatarishi

Wasifu

Flora E. Nyanana ni Mchumi aliyebobea katika usimamizi wa miji na mipango mkakati. Akiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 10 katika sekta ya umma, amejipambanua kama kiongozi katika mipango na uratibu. Weledi wake kitaaluma umechangiwa na Shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Usimamizi na Maendeleo ya Miji kutoka Chuo Kikuu cha Erasmus Rotterdam nchini Uholanzi, pamoja na Shahada ya Uzamili katika Ufuatiliaji na Tathmini.

Katika kipindi chote cha utumishi wake, Flora amedhihirisha uwezo mkubwa wa kusimamia miradi ya serikali na kuboresha utendaji wa mamlaka za Serikali za Mitaa. Uzoefu wake mkubwa wa uongozi unajumuisha kuhudumu kama Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu katika Manispaa ya Kigamboni, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, ambapo amekuwa akioanisha malengo ya Manispaa na ukuaji wa kimkakati pamoja na utoaji wa huduma kwa ufanisi.