Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
Huduma za ATM katika Vituo Vikuu

Wakala umetenga nafasi kwaajili ya ufungaji na uendeshaji wa mashine za kutolea Fedha hususani kwenye vituo vikuu. Kwa sasa kuna Mashine moja ya kutolea fedha katika Kituo Kikuu cha Gerezani na bado Wakala unakaribisha Wadau wengine kutumia fursa hii. Lengo ni kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa abiria wa Mabasi Yaendayo Haraka na watu wengine.