Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
Ujumbe wa Mwenyekiti wa Board

Nipende kuchukuwa nafasi hii kukushukuru kwa kutembelea tovuti yetu.

Lengo la Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka ni kuwarahisishia wakazi wa jiji la Dar es salaam kusafiri kwa haraka, wakitumia Mabasi ya kisasa yenye viwango vya kimataifa kwa gharama nafuu. Matarajio ya wakala ni kuwa na jiji la kisasa linaloendeshwa kidijitali, hivyo kila mtumishi wetu anafanya jitihada za kuhakikisha wateja wetu wanaamini kwenye maono hayo.

Ninaamini kuwa hakuna njia ya mkato katika kufikia malengo ya taasisi kibiashara pasipo uwepo wa uadilifu, usalama na kutegemewa, uendelevu, kulenga wateja, kufanya kazi kwa pamoja n.k. Ninaamini sana katika kufanya kazi kwa bidii, ili kufikia Malengo yaliyokusudiwa.

Pamoja na tafakuri yetu ya utekelezaji wa Awamu Sita za Mradi wa DART kwa Wakazi wa Dar es salaam huku ujenzi wa Awamu ya Kwanza ukiwa  umekamilika na huduma kutolewa. Tunazingatia kuboresha miundombinu yetu kufikia viwango vya kimataifa, uwekezaji kwa watu sahihi, teknolojia, kuboresha vyanzo vyetu vya mapato na hivyo kufanya Wakala kuwa na nguvu kiuchumi.

DART ina suluhu na mapendekezo sahihi ya ushirikiano wa sekta ya umma na sekta binafsi katikan nyanja ya usafirishaji, ambapo tunaamini katika uhusiano shirikishi utakaokuza uchumi wa Taifa letu kupitia miradi ya ujenzi wa miundombinu, uendeshaji wa mradi wa mabasi pamoja na fursa nyingine za kibiashara na masoko zinazopatikana katika ushoroba wa mabasi yaendayo haraka.

Kwa mara nyingine tena, asante kwa kutembelea tovuti yetu na kuchukua muda wako kufahamu kuhusu huduma za Wakala wa Mabasi yaendayo haraka.

 Asante

Florens M.Turuka PhD.

Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa Wakala