Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
Mfumo wa DART Awamu ya Pili

Tarehe 30 Septemba, 2015 Africa Development Bank iliidhinsha mkopo wa kusaidia juhudi za serikali ya Tanzania kupunguza msongamano wa usafiri jijini Dar es Salaam ambapo tarehe 23 Oktoba, 2015 serikali ya Tanzania imetiliana saini na benki hiyo kugharimia mradi.

Hivi sasa Washauri wa Usimamizi wapo kwenye eneo la mradi ambao ni M/s BOTEK Bosphorus Technical Consulting Corporation ya Turkey kwa kushirikiana na Apex Engineering Co. Ltd ya Tanzania kwaajili ya ujenzi wa barabara na Interconsult Tanzania Limited kwaajili ya majengo.

Mchakato wa kuwapata wakandarasi kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya awamu ya pili ya DARTunaendelea na zabuni ya ujenzi wa barabara imetangazwa mwezi Mei 2018 na tarehe ya mwisho ya kuwasilisha ni tarehe 2 Julai, 2018 wakati tathmini ya zabuni kwaajili ya majengo inaendelea.