Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

"Usafiri wa Umma Nadhifu"

DART Logo
KUSITISHA VIBALI VYOTE VYA KUPITA KWENYE BARABARA ZA BRT
10 Dec, 2025 Pakua

 TAARIFA KWA UMMA

 

 

YAH: KUSITISHA VIBALI VYOTE VYA KUPITA KWENYE BARABARA ZA BRT

 

 

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), unautaarifu umma kuwa kuanzia sasa, vyombo vyote vya usafiri isipokuwa Mabasi Yaendayo Haraka haviruhusiwi kutumia njia maalum za Mabasi Yaendayo Haraka (BRT).

 

DART inasisitiza kuwa vibali vyote vilivyowahi kutolewa vimesitishwa kuanzia tarehe tajwa. Doria na udhibiti vitaimarishwa ili kuhakikisha agizo hili linazingatiwa. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka agizo hilo.

 

Aidha, DART inatoa wito kwa wananchi wote kushirikiana kulinda miundombinu ya BRT.

 

 

 

 

 

Imetolewa na:

 

Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka-DART

 

10 Desemba 2025